Jumanne , 21st Nov , 2017

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA), Patrick Ole Sosopi amesema kwamba kuondoka kwa Mwenyekiti wa baraza hilo Patrobas Katambi ndani ya Chama hicho hakijawateteresha na kudai kwamba Katambi hakuwa mkubwa kuliko Chama chao.

Akizungumza masaa machache baada ya Mwenenyekiti wa Baraza hilo kuhamia CHADEMA, Ole Sosopi amesema kwamba Patrobasi hakuwa Bavicha kwani aliingia ndani ya chama hivyo akiwa hana umaarufu hivyo kuondoka kwake kusiwavunje moyo vijana vingine na kusisitiza kwamba bado baraza hilo la vijana lipo imara.

"Patrobas siyo Bavicha, ila yeye alikuwa sehemu ya Bavicha. Bavicha ipo imara na hii ni taasisi. Na Patrobasi kuondoka Chadema siyo jambo geni, ni jambo la kawaida kama jinsi viongozi wengine wavyotoka chama kimoja kwenda kikingine. Tunamtakia kila la kheri huko alipokwenda. Vijana wetu waendelee kuiwa busy kufanya kampeni kwa ajili ya uchaguzi na wasihangaike na habari za Patrobas". Ole Sosopi

Ameongeza kwamba "Ndani ya Chadema hakuna mtu maarufu isipokuwa Patrobas alipata umaarufu alipokuwa ndani ya Chama na ameondoka, hivyo Chama kitaendelea kuwa imara siyo kwa ajili ya mtu mmoja. Kupitia uchaguzi huu mdogo tunapaswa kutuma meseji kwa CCM na yeye Katambi  hivyo vijana msihamishwe na hili jambo mkaacha kuendeleza kampeni". Ole Sosopi

Aidha aeongeza kwamba kitendo cha Patrobas kuhamia CCM ni usaliti ambao ameudhihirisha kwa watanzania na wanachama kuungana na watu au serikali ambayo imeshindwa kumbaini nani aliyempiga risasi mwanasheria mwenzake Tundu Lissu.

Ameongeza kwamba kinachofanyika na CCM siyo siasa bali ni 'Project' inayofanyika kushawishi watu waone kwamba CCM imebadilika lakini ukweli ni kwamba "CCM ni ileile na madudu yake ni yaleyale kwa zaidi ya mika 50 nawashauri wafanye siasa zinazohgusa wananchi"