Waziri Ummy Mwalimu akizungumza na wanahabari
Ummy amebainisha hayo leo wakati alipokuwa anazungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam na kusema wananchi wasiwe na hofu ila wanapaswa kuchukua tahadhari huku akisisitiza kuwa wameweka kifaa maalum 'register' ambacho kitawalazimu wasafiri wote kujaza wakiwa wanakwenda katika nchi ya DRC na pindi wakiwa wanatoka huko kuingia nchini.
"Hadi sasa hakuna mgonjwa hata mmoja wa Ebola wala mwenye virusi Tanzania, tumechukua tahadhari katika mikoa yote inayopakana na nchi ya Congo DRC. Wasafiri wote wanaotoka DRC wakifika Tanzania lazima waandikishwe kimaalum ili kufuatiliwe kama huko alikotoka hali ikoje na kama hana virusi nyemelezi. Tunawaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza katika kuwapima wasafiri wote kwenye mipaka yetu na Congo DRC" alisema Ummy.
Aidha, Ummy amesema serikali imeagiza mashine nne za nyongeza kutoka nje ya nchi ili kuongeza nguvu ya upimaji wa virusi vya ugonjwa huo.