Jumatano , 10th Aug , 2022

China imeapa kutovumilia vitendo vya kutaka kujitenga Taiwan na kusisitiza kwamba itakichukua kwa nguvu kisiwa hicho kinachojitawala chenyewe pale itakapobidi 

Onyo hilo limetolewa baada ya siku kadhaa za luteka za kijeshi karibu na kisiwa hicho zilizochochewa na ziara ya Spika wa Bunge la Marekani Nancy Pelosi. 

Ofisi ya China inayohusika na masuala ya Taiwan imetoa leo waraka unaoeleza jinsi inavyodhamiria kukinyakua kisiwa hicho kupitia  shinikizo la kijeshi

Waraka huo umesema China iko tayari kutengeneza nafasi kubwa ya kuungana upya, lakini haitaacha nafasi ya vitendo vya kujitenga kwa njia yoyote ile

China mara ya mwisho ilitoa waraka wa aina hiyo kuhusu Taiwan mwaka wa 2000. Taarifa za hivi punde zimearifu kuwa China imetangaza kumalizika kwa mazoezi yake ya kijeshi  kuizunguka Taiwan