Majaliwa alisema hayo leo alipotembelea kiwanda cha kutengeneza sabuni kilichoko Kibaha na kiwanda cha kutengeneza vigae kilichoko Pingo halmashauri ya Chalinze.
Amesema vijana wanatakiwa kuonyesha uwezo mkubwa wa kufanya kazi ili waweze kupata ajira kwani katika viwanda ajira zinapatikana kwa watu wenye uwezo tofauti, wasomi na wasio wasomi.
Majaliwa pia amewagiza viongozi wa Halmashauri ya Kibaha na Chalinze kuhakikisha wanatengeneza miundombinu yote ya barabara pamoja na kutenga maeneo ya viwanda ili kuwavutia wawekezaji.
Mh. Majaliwa amesema Serikali itahakikisha inasaidia kutatua changamoto zinazojitokeza ikiwemo ukosefu wa maji katika mji wa Chalinze pia kuwezesha jeshi la zima moto kuwa na vituo vya kutosha vya kuzimia moto , sambamba na vitendea kazi ili kulinda maisha ya watu na mali pindi moto unapoweza kutokea.