Jaji Mutungi ametoa kauli hiyo leo Jijini Dar es Salaam alipokutana na Baraza la Vyama nchini ambao walikuwa wanajadiliana namna ya kupata muafaka wa kutatua changamoto ambazo zinaendelea kujitokeza ndani ya baadhi ya vyama.
Wakati huohuo Jaji Mutungi amesema ofisi yake imesogeza mbele mkutano wa baraza uliopangwa kufanyika tarehe 29 mwezi huu hadi tarehe 3 na 4 Oktoba.