Jumatano , 20th Sep , 2017

Jeshi la Polisi limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wakazi wa bonde la mto Msimbazi waliokuwa wakipinga kubomolewa makazi yao, na kuwakamata watu takriban 20 wakihusika kufanya vurugu hizo.

Tukio hilo limetokea Septemba 20, 2017  kwenye bomoabomoa ambayo inatekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, yenye lengo la kuandaa eneo ili kupisha mradi mkubwa wa majitaka katika manispaa hiyo.

Wakazi wa eneo hilo wamelalamikia zoezi hilo na kuiomba serikali kuwaonea huruma kwani hawana mahali pengine kwa kwenda kujisitiri.                        

Pamoja na hayo pia eneo hilo la Jangwani lilishapigwa marufuku kwa wananchi kujengwa makazi, kwani ni eneo hatarishi kutokana na kuwa kwenye mkondo wa mto Msimbazi ambao nyakati za masika hufurika.

Gari la mwendokasi likiwa limevunjwa kioo katika vurugu hizo
Kituo cha mwendokasi kikiwa kimeharibiwa
Kituo cha mwendokasi kikiwa kimevunjwa vioo