Jumapili , 20th Sep , 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli  amemtaka Waziri wa TAMISEMI kumpatia fedha Meneja wa TARURA Wilaya ya uvinza shilingi za kitanzania bilioni tano kwa ajili ya utengenezaji wa barabara ya uvinza mkoani kigoma.

Rais Magufuli na Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo

Agizo hilo amelitoa hii leo Septemba 20,2020 kwa njia ya simu wakati akiongea na wananchi  njiani kuelekea mkoa wa Tabora ambapo amesema  fedha hizo ambazo zitatolewa ni kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa barabara ya kilometa kumi kwenda uvinza.

"Mheshimiwa Jafo, niko Uvinza nimeshatoa maagizo TARURA waletee bilioni  tano wamalize kilometa zote kumi za kwenda Uvinza, kesho utekeleze na umletee Meneja wa TARURA hizo bilioni tano ashughulikie hii barabara aweke wakandarasi  nataka lami wananchi wa'enjoy'", amesema Dkt. Magufuli.

"Zote tengeneza nataka siku nikija hapa  jiwe la msingi  nataka nije nikute pamewekwa lami hadi uvinza  mjini  nataka nikalale uvinza", ameongeza.

Aidha Rais Magufuli amesema kuwa anafahamu kwamba Mkoa huo wa Kigoma hasa wilaya uvinza unakabiliwa na tatizo la umeme tangu nchi imepata uhuru  ambapo ameahidi  kulishughulikia suala hilo.