Alhamisi , 25th Feb , 2021

Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, ameufagilia na kuomba apigiwe wimbo ulioimbwa na Professor Jay na Stamina, wenye ujumbe unaomsema baba aliyeshindwa kutimiza majukumu yake kwa mtoto unaoitwa Baba.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli, akiutazama wimbo wa Professor Jay na Stamina

Rais Dk. Magufuli amebainisha kuvutiwa na mashairi ya wimbo huo leo Februari 25, 2021, Jijini Dar es Salaam, wakati akizindua jengo la Jitegemee na Africa Magic Group Limited.

"Mimi nataka muziki mmoja nafikiri umepigwa na Professor Jay, unazungumzia juu ya mtu aliyekwenda kumsema baba yake, akasema nazungumza na wewe sijui unaitwaje ?, huu wimbo una message (ujumbe)," alisema Rais Dkt.magufuli.