Katibu Mkuu Wizara ya Afya Profesa Mabula Mchembe
Profesa Mabula, ameyasema hayo hii leo Septemba 17,2020, wakati akifanya uzinduzi wa vitambulisho 524 vya wakaguzi vilivyoboreshwa, uliofanyika katika Ofisi za TMDA Jijini Mwanza, ambapo amesema mamlaka hiyo inajukumu la kufuatilia wakaguzi ili kumlinda mwananchi na kuhakikisha bidhaa zinakuwa bora kwa matumizi ya binadamu.
"Sera yetu ya wizara kama mnavyoifahamu ni kuhakikisha bidhaa aina ya dawa pamoja na vifaa tiba vinatumika hapa nchini kwa ubora na vikiwa vimethibitishwa usalama wake ili kuwalinda watumiaji", amesema Profesa Mabula.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Adam Fimbo amesema, uwepo wa vitambulisho vilivyoboreshwa utatatua changamoto ya watu wanaojitokeza ambao wamekuwa wakitengeneza vitambulisho bandia kwa nia ya kuwalaghai wananchi.