Waziri Balozi Dkt. Pindi Chana ameyasema hayo, Wilayani Makete mara baada ya . Rais Samia kutaka kujua hali ya mgogoro wa mpaka kati ya Hifadhi ya Kitulo na wananchi wanaopakana na hifadhi hiyo.
Aidha, ameeleza kuwa licha ya kazi kubwa inayoendelea kufanywa na kamati inayojumuisha Mawaziri 8 ya kutatua migogoro, Wizara anayoiongoza ipo katika hatua nzuri ya kutafuta ufumbuzi wa kudumu ikiwashirikisha Wananchi na Serikali ya Wilaya.
Waziri Balozi Dkt. Chana ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha wanazingatia na kuheshimu makubaliano na mipaka iliyowekwa ili kuepuka kuibua migogoro mipya inayodhoofisha shughuli za uhifadhi wa Rasilimali adhimu za Urithi wa Utalii.
Rais Samia Suluhu Hassan yupo mkoani Njombe kwa ziara ya kikazi ya Siku mbili ambapo moja ya mambo aliyoyafanya ni pamoja na kufungua Barabara ya Makete Njombe.