Jumatano , 6th Jul , 2022

Yamefanyika maziko ya pamoja ya vijana 21 waliopoteza maisha kwenye klabu moja ya usiku nchini Afrika Kusini wiki iliyopita, huku sababu ya vifo vyao ikiendelea kuchunguzwa.

Miongoni mwa wageni 3,000  wakiwemo viongozi mbalimbali  wa serikali, ndugu jamaa na marafiki waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa.

Vijana waliopoteza maisha wana umri wa kati ya miaka  13-17 .

Hakuna taarifa  rasmi za chanzo sahihi cha vifo vya vijana hao 21, ambao walifariki dunia wakati wakisherehekea kumaliza mitihani yao ya mwisho kwenye klabu hiyo ya usiku. 

Wafuatiliaji wa mambo nchini humo  wanasema kuwa huenda vijana hao walikosa hewa ama kuvuta hewa chafu yenye sumu ambayo huenda ilisababisha vifo vyao, lakini mpaka sasa hakuna taarifa rasmi.  

Janga hilo limeibua upya maswali kuhusu uwepo wa klabu za usiku nchini humo, ikiwemo kuanza kufuatilia leseni na vibali mbalimbali vya uwepo wa maeneo hayo ya burudani., huku vilabu vya usiku kwenye maeneo hayo vikifungwa kufuatia tukio hilo.