Alhamisi , 12th Jan , 2017

Mahakama nchini Kenya imetoa hati ya kukamatwa viongozi wa chama cha madaktari, kutokana na kutokuwepo mahakamani wakati ikitolewa hukumu iliyowatia hatiani ya kuingilia maamuzi ya mahakama

Mgomo wa madaktari nchini Kenya

 

Uamuzi huo wa mahakama umetolewa wakati, serikali ya kitaifa nchini Kenya ikiendelea na jitihada za kufanya majadiliano na madaktari ili kumaliza mgomo wao uliodumaza kabisa huduma za afya katika sekta ya umma.