Awali Baraka Chelela ambaye ni Kaimu mhifadhi wa msitu wa mbizi akiongea katika kufunga Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa mda wa siku nne kuwa ni pamoja na kuishirikisha jamii katika kulinda mazingira ya misitu huku Konstable Joston Seme kutoka kitengo cha Elimu na mafunzo kwa Umma kutoka jeshi la zimaoto na uokoaji akitoa wito kwa wananchi kufatilia mafunzo yanayotolewa na jeshi hilo ili kuepukana na majanga.
Kwa upande wake baadhi ya vijana walioshiriki mafunzo hayo ya kuthibiti na kuzuia majanga ya moto yaliyoenda sambamba na zoezi la kuchoma msitu na kuthibiti moto wakaeleza manufaa wanayoyapata kupitia msitu wa mbizi.