Jumamosi , 18th Nov , 2017

Msanii mkongwe wa muzuki wa kizazi kipya, Selemani Msindi marufu kwa jina la Afande Sele, ameweka wazi juu ya chuki aliyonayo kwa tasnia ya filamu bongo (bongo movie).

Akiongea na Planet Bongo ya East Africa Radio, Afande Sele amesema hawachukii wasanii wa bongo movie, bali huchukia tabia zao chafu ambazo zinaharibu Tasnia.

Afande Sele ameendelea kwa kusema kwamba wasanii wa bongo movie wana tabia chafu hasa za kuwanyanyasa wanawake kwa kuwatumikisha kingono, huku akimtolea mfano muigizaji Elizabeth Michael (Lulu) ambaye amefungwa.

Msikilize hapa chini