Alhamisi , 23rd Oct , 2014

Msanii Akili The Brain amesema kuwa utaratibu wake kwa sasa ni kutoa ngoma zisizozidi Mbili kila mwaka licha ya kumiliki studio yake mwenyewe ikiwa ndio sababu ya watu kuona kama huwa haishi nchini na anakuwa kimya sana.

msanii wa muziki wa bongofleva nchini Tanzania Akil The Brain

Akili ameongea na eNewz kuwa kwa kawaida ngoma zake huwa zinakaa studio muda mrefu ili kutoa nafasi kwa kazi iliyotangulia na pia kutoa muda wa kurekebisha rekodi hizo vizuri kabla ya kuziachia kwa mashabiki.

Mkali huyo wa miondoko ya Bongo Bhangra kwa sasa anatamba na ngoma yake inayokwenda kwa jina Habibty ambayo amemshirikisha msanii mkali Saraha.