Ijumaa , 30th Jan , 2015

Katika kuelekea kipindi cha Uchaguzi Mkuu nchini Tanzania, amani ikiwa ni somo kubwa linalohubiriwa kwa wananchi kila ngazi, nyota wa muziki Ali Kiba, amesema kuwa yeye pamoja na sanaa yake amekuwa kati ya wadau wanaolitilia mkazo suala hili.

Msanii wa muziki wa bongo fleva nchini, Ali Kiba

Ali Kiba amesema kuwa, Tanzania imekuwa ni nchi ambayo inatambulika kwa amani, changamoto kubwa ikiwa ipo katika nchi za jirani ambapo amekwishaenda si tu kwa kutoa burudani, bali kwa kuhamasisha amani kwa wapenzi wa kazi zake.