Ommy Dimpoz
Akiongea kupitia eNEWZ ya EATV, Ommy amesema kwa sasa anaishi Mikocheni Dar es Salaam na hajawahi kuwekwa ndani na mwanamke yeyote kwa kuwa anasema mpenzi wake wa sasa ni mchina na hajawahi kuwa na mahusiano na mwanamke wa kizungu na kwamba hizo ni story za watu ambao waliamua kuvumisha.
Hata hivyo Ommy amesema kwa sasa anajenga nyumba yake maeneo ya Mbezi na Kigambona hivyo hana nyumba ambayo amepangisha au kupangishiwa Mbezi na mambo yatakapokuwa wazi atamuweka wazi mpenzi wake.