Gabo Zigamba
Gabo ambaye anatamba na filamu yake fupi ‘Kisogo’, ambayo ameshirikiana na Wema Sepetu, alisema ujio wa kazi hiyo mpya ni kutekeleza kwa vitendo mpango wake wa kuleta mapinduzi katika tasnia hiyo.
Gabo ni msanii pekee wa kiume anayetazamwa na mashabiki wengi wa filamu za hapa nchini na kuonekana kuwa anaweza kuziba pengo la marehemu Steven Kanumba.