Alhamisi , 18th Feb , 2021

CEO wa Konde Gang Music Harmonize amesema kutokana na umbali wa mapenzi  kati yake na aliyekuwa mke wake Sarah ndiyo ilisababisha kuchepuka na mwanamke mwengine ambaye amezaa naye mtoto mmoja wa kike.

Picha ya msanii Harmonize akiwa studio za East Africa Radio

Akifichua siri hiyo msanii Harmonize ameeleza kuwa "Ishu za Sarah hakuzinisumbua na sio kama nilikuwa simpendi, yeye  alisafiri akakaa kama miezi mitatu kwa sababu alikuwa na matatizo ya kifamilia kwao, kwa hiyo nikajikuta nime-date na mwanamke mwingine kutokana na ile love distance"

"Yule mwanamke akapata ujauzito na tukasema iwe siri na nilikuwa nahudumia kila kitu, sasa nikasema nitakaa hivi mpaka lini, nikamfuata mpenzi wangu 'Sarah' kumueleza matatizo yaliyotokea kibinaadam lakini ilikuwa mtihani kwake, so tukaishia hapo" ameongeza 

Zaidi tazama hapa chini kwenye video.