Jumanne , 27th Sep , 2016

Msanii Joslin ambaye aliwahi kufanya vizuri kwenye muziki wa Bongo Fleva ametangaza kurudi tena kwenye muziki baada ya kuanza kufanya video ya wimbo wake mpya 'Only you' ambao anatarajia kuuachia siku za usoni.

Joslin (Kushoto)

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Joslin aliandika juu ya ujio wake huo mpya "Yeah...the return of Joslin...(ndoto yao) " pia video Queen ambaye anamefanya video hiyo Proyanca Michael alifunga na kusema kuwa anatambua watu wamemkumbuka sana hivyo ni wakati wake kurudi na ngoma hiyo mpya 'Only You'.

"The Return of Joslin I know you have missed him a lot but now He's back with a new hit song 'ONLY YOU' soon it will be released stay tune and let's support him and God bless you all" aliandika Proyanca Michael