Msanii Mo Music kwenye picha kubwa, picha ndogo ni Nandy ambaye amevalia mavazi ya kiganga
Mo Music amesema alienda kwa mganga kwa sababu aling'atwa na nyoka mguuni hivyo akaenda kupatiwa tiba pia alishawahi kumpeleka mtu mwingine ambaye alikuwa na matatizo ya akili.
"Nimewahi kwenda kwa mganga ila nilikuwa naumwa mguu na niling'atwa na nyoka, karibia asilimia 90 ya wasanii wote wanamjua mganga lakini kikubwa ni kuangalia juhudi zako, pia niliwahi kwenda kwa ajili ya kumpeleka mtu ambaye alikuwa ana matatizo ya akili, sisi tunaamini kwenye u-Afrika bana" amesema Mo Music
Zaidi tazama hapa chini.