Alhamisi , 19th Jan , 2017

Mwana hip hop wa Bongo Nash MC a.k.a Maalim Nash amefunguka na kuwataka baadhi ya watanzania wanaoishi nje ya Tanzania hususani Afrika Kusini kuacha tabia ya kuuana kwani kitendo hicho kinazidi kupoteza ndugu na kwamba huo ni unyama.

Nash MC

 

Nash MC amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Facebook na kudai karibu kila mwezi wanapata taarifa juu ya Watanzania kupotezana duniani hivyo amewataka raia hao kujikita kwenye utafutaji wa maisha ili tusonge mbele ila si kutoana uhai kwani si jambo jema.

"Washkaji zetu mnaoishi Afrika Kusini mnatusikitisha sana ndugu zenu hapa bongo maana haipiti mwezi utasikia ndugu zetu mmeuana. Sio poa mabaharia, fanyeni tathmini wenetu wangapi washaondoka duniani kwa mtindo huo? Pambaneni na maisha tusonge mbele. Mtanzania sio poa kumdondosha mtanzania mwenzake". Nash MC