Jumatatu , 22nd Dec , 2014

Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania, Ney wa Mitego ambaye pia amekuwa ni machachari katika kutimiza amri ya kuujaza ulimwengu, ameweka wazi kuwa kati ya mambo makubwa anayoyahofia katika maisha yake, mojawapo ni ishu nzima ya kuoa.

Msanii wa miondoko ya bongofleva Ney Wa Mitego

Ney amesema kuwa, kwa upande wake binafsi akifikiria anakosa sababu hasa ya hofu hii, ila kuoa ni kitu ambacho kinamtoa jasho pale anapokifikiria wazo hilo.