Akizungumza na eNewz ya East Africa Tv Meneja huyo ameeleza kuwa "Wasanii hawajawahi kunifilisi kwanza sanaa ya muziki nilikuwa nafanya kama starehe kwangu na ukiangalia asili ya watu wa Musoma wengi wao wanafanya muziki kwa starehe na sio biashara kwa sababu mimi hakuna pesa ya muziki ambayo nimewahi kula ila nimetumia pesa nyingi kusimamia muziki"
Aidha Ostadh Juma na Musoma ameongeza kusema sio kwamba amefilisika ndiyo amehamia Tanga bali ameenda kwa ajili ya masomo, pia kabla ya kuja Dar Es Salaam alipitia mkoani humo na ndipo alipopewa jina la Ostadh.
Zaidi mtazame hapa chini akizingumzia kuhusiana na hilo