Jumanne , 13th Oct , 2015

Mtayarishaji maarufu wa muziki hapa nchini kutoka studio za Combination sound, Man water, amesema watu maarufu hususani wasanii, wanakuwa na wakati mgumu sana katika kumpata mtu sahihi wa kuwa naye kwenye mahusino.

Man Water ameyasema hayo kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa radio, na kusema kwamba mara nyingi wasanii wa kiume wanapata wakati mgumu wa kutambua yupi ana mapenzi ya kweli.

"Unajua sisi wasanii, producers, watu ambao famous tunakuwaga na changamoto sana inapokuja kwenye suala la mahusiano, mapenzi, mimi nilikuwa sijui who is the right person, yani napata marafiki wengi wa kike kiurahisi tu, lakini nashindwa kujua hawa wanampenda John au wanampenda Man Water!?, sababu hata mahusiano yenyewe yanaanzakiurahisi na yanavunjika kiurahisi", alisema Man Water.

Man water aliendelea kwa kusema kwamba kitendo hicho mara nyingi wanaume ndiyo wanakuwa waathirika wakubwa kuliko wanawake, kwani wao hujikuta wamependa na wenzao wakiwa wamefuata umaarufu wao.

"Kwa upande wa dada zetu sidhani kama wanaumiaga, ila upande wa mwanaume inaonekana anaumia kwa sababu ye anakuwa ameanza kupenda, lakini kumbe wewe umependa ile fame