Maganga amebainisha hayo baada ya kuwepo mvutano wa muda mrefu kati ya Kagera Sugar na Azam FC ambapo kila timu ilikuwa inavutia upande wake, hatimaye mvutano huo umepata suluhisho.
"Jana tulifanya kikao na Kagera Sugar na mwisho tumefikia muafaka kuhusiana na suala hilo na sasa Mbaraka ni mchezaji halali wa Azam FC. Lakini bado hatujaanza kumtumia kwa sababu aliumia akiwa na timu ya Taifa hivyo bado yupo chini ya uangalizi wa daktari na anafanya mazoezi mepesi mepesi ili baadaye aweze kujiunga na kikosi kwa ajili ya mechi za Ligi" alisema Maganga.
Mshambuliaji Mbaraka Yusuph.
Pamoja na hayo, Maganga amesema timu ya Kagera Sugar wametoa barua maalum ya kumuachia Mbaraka aitumikie Azam FC kwa sasa.
Mbaraka Yusuph amesaini kandarasi ya miaka miwili kuwatumikia wanarambaramba hao wa Vingunguti.