Domayo amejiunga na Klabu hiyo akiwa mchezaji huru, baada ya kuachwa na Azam FC mwishoni mwa msimu uliopita 2021/22.
Domayo ametambulishwa rasmi Klabuni hapo kupitia Kurasa na Mitandao ya Kijamii ya Namungo FC, huku taarifa hiyo ikiandikwa: #WelcomeTosouthernkillers
Karibu kwenye Familia ya Namungo Fc Frank Raymond Domayo
Kiungo huyo anakuwa mchezaji wa pili kutambulishwa Namungo FC katika kipindi hiki cha Dirisha Dogo la Usajili, akitanguliwa na Mshambuliaji kutoka nchini Ghana Stephen Sey.
Sey aliwahi kuitumikia Namungo FC msimu wa 2020/21 kabla ya kuondoka, baada ya kusajiliwa na Klabu ya Eastern Company SC ya nchini Misri.