Alhamisi , 8th Dec , 2016

Siku moja baada ya kutangaza kutundika groves, bondia bingwa wa zamani wa uzito wa kati Mtanzania Francis Cheka 'amebadili gia angani'.

Francis Cheka

Cheka amechukua uamuzi huo wa kubadilisha maamuzi yake ya awali baada ya hii leo kukabidhiwa barua ya kuombea viza ya kwenda India ambako atapambana na bondia wa nchi hiyo katikati ya mwezi huu.

Cheka alitangaza kustaafu ndondi kufuatia kukerwa na baadhi ya watu aliodai kutaka kumkwamisha katika safari za kwenda nje kucheza mapambano ya kimataifa.