Alhamisi , 21st Oct , 2021

Timu ya kikapu ya Kurasini Heats, imeanza rasmi mazoezi yakujiweka sawa kuelekea michezo ya hatua ya Awali ya kufuzu fainali za Basketball Africa League zitakazofanyika Uwanja wa ndani wa Taifa kwanzia Oktoba 26-31 jijini Dar es salaam.

(Rais wa Chama cha Mpira wa kikapu nchini, Phares Magesa akiw ana mabingwa wa kikapu taifa, Kurasini Heat.)

Mashindano hayo yatakayokutanisha timu nane ambao Ni mabingwa katika Ligi zao  barani Afrika kupa nafasi ya kuwa miongoni mwa timu 16 zitakazopata nafasi ya kushiriki Basketball Africa League, Ligi ambayo ipo chini ya usimamizi wa NBA, ambapo kwa mwaka mwingine tena Rwanda watakuuwa wenyeji Mwakani 2022.

Kurasini Heats ambao Ni mabingwa wa Taifa wa Kikapu Maarufu Kama NBL kwa mwaka 2020 wataiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya mwaka huu baada ya kutoshiriki kwenye michuano iliyofanyika mwakani baada ya kufanyika Kigali kwa mafanikio makubwa mwaka huu.

Licha ya kutofanya vizuri kwenye Msimu huu wa Ligi ya mkoa, RBA Dar es salaam, Heats wanaingia Kambini kuhakikisha wanaiwakilisha nchi vyema kwa Mara ya kwanza na kwasasa wanajizatiti kufanya usajili wenye tija baada ya kupoteza wachezaji wake mahiri Kama Amin Mkosa aliyejiunga na Braves ya Malawi.

Timu kumi na mbili za msimu wa uzinduzi wa BAL zililazimika kufuzu katika mashindano yao ya ndani ili kuweza kucheza kwenye ligi, sawa na mashindano mengine yaliyopangwa na FIBA. mwakani Timu sita zinafuzu moja kwa moja kama mabingwa wa nyumbani; washindi sita wa mashindano ya kufuzu wanastahili pia.

Kulingana na kanuni za BAL, FIBA ​​ilitangaza kuwa mabingwa wa kitaifa wa Angola, Misri, Morocco, Nigeria, Senegal na Tunisia wamehitimu moja kwa moja kwa msimu wa kawaida na kufuzu kwa Fainali za mwakani

Mnamo 22 Mei 2020, Petro de Luanda alitangazwa kama timu ya kwanza kufuzu kwa msimu wa 2021 BAL. FAB ya Angola ilikuwa imeachana na msimu kutokana na janga la COVID-19 na kuipatia timu hiyo nafasi bila kuiita kama mabingwa.