Salum Aboubakar(Sureboy) wa Azam (Kulia ) na Feisal Salum wa Yanga (Kushoto) katika kipute cha VPL.
SOKOINE -MBEYA
Ihefu ambao ni wageni katika ligi watakua katika Uwanja wao wa nyumbani kwa mara ya tatu mfululizo .
Kikosi cha Ihefu ambacho kinanolewa na Kocha Maka Mwalwisi, kilifungua dimba dhidi ya Mabingwa watetezi Simba,na walipoteza kwa bao 2-1, kabla ya kuinyuka Ruvu Shooting bao 1-0.
Hadi sasa Ihefu wapo nafasi ya 7 kwenye msimamo wa ligi wakiwa na alama 3,na watakabiliana na Mtibwa Sugar ambao wanawania ushindi wa kwanza msimu huu baada ya kuambulia alama 2 katika mechi 2 walizocheza dhidi ya Ruvu Shooting waliyotoka suluhu na sare ya bao 1-1 na Simba.
USHIRIKA-KILIMANJARO
Polisi Tanzania wao watacheza mechi yao ya kwanza katika Uwanja wao wa nyumbani baada ya kucheza mechi 2 ugenini dhidi ya Azam Fc waliyopoteza kwa bao 1-0 kabla ya kuiduwaza Namungo nyumbani kwao kwa kuwanyuka bao 1-0.
Wakiwa nafasi ya 8 na alama zao 3,Polisi ambayo inanolewa na Kocha Malale Hamsini,watakabiliana na JKT Tanzania ambao katika mchezo uliopita walikubali kipigo cha bao 2-0 kutoka kwa Dodoma Jiji .
Kocha Mohamed Abdallah Baresi wa JKT Tanzania atashuka dimbani leo akiwa na hazina ya alama 3 alizozivuna ugenini katika mechi ya ufunguzi walipoifunga Kagera Sugar bao 1-0 huko Kaitaba.
JKT Tanzania wanakamata nafasi ya 10 katika msimamo wakiwa wamekusanya alama 3 katika mechi 2 walizocheza.