Jumatatu , 18th Sep , 2017

Kocha wa Manchester United Jose Mourinho amesema anaamini ipo siku nyota wa zamani wa timu hiyo Wayne Rooney atarejea klabuni hapo.

Mourinho amesema hayo mbele ya waandishi wa habari alipoulizwa kuhusu mapokezi ya Rooney kwenye mchezo wa jana kati ya Manchester United dhidi ya Everton ambapo mashabiki walimpokea nyota huyo kwa shangwe nyingi.

"Rooney hana tatizo na timu wala mimi sina tatizo na Rooney ndio mana tumesalimiana kwa furaha, naamini siku moja atarejea maana hapa ni nyumbani kwake hata mashabiki wamempokea vizuri"' amesema Mourinho.

Rooney jana alirejea kwa mara ya kwanza kwenye uwanja wa Old Trafold tangu aondoke kwenye dirisha la usajili lililopita ambapo alirudi kwenye timu yake iliyomkuza ya Everton na jana ilikumbana na kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa United.

Rooney ndiye mfungaji bora wa muda wote wa klabu ya Manchester United akiwa na mabao 253.