Ijumaa , 24th Feb , 2017

Kamati ya Waamuzi imemtangaza rasmi Mathew Akrama kutoka Mwanza kuwa mwamuzi wa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba na Yanga, siku ya Jumamosi Jumamosi Februari 25.

Mathew Akrama

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Salum Umande Chama ndiye aliyetoa taarfa hiyo leo, ikiwa ni siku moja baada ya Shirikisho la Soka nchini (TFF) kupitia kwa msemaji wake Alfred Lucas kudai kuwa jina la mwamuzi huyo lingekuwa siri hadi siku ya mchezo.