Semtawa ambaye alikuwa kiungo wa Coastal Union ambaye imeshuka daraja kwa msimu uliopita, kitaaluma ni daktari.
Semtawa anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa Mbeya City wiki hii, baada ya mwanzoni mwa wiki kusajiliwa beki wa Yanga, Rajab Zahir aliyekuwa anacheza kwa mkopo Stand United.