Alhamisi , 21st Oct , 2021

Klabu ya Simba imezindua kauli mbiu yao ‘’It is not over, kazi iendelee’’ kuelekea mchezo wao wa hatua ya pili katika michuano ya klabu bingwa Afrika siku ya Jumapili dhidi ya Jwaneng Galaxy F.C ya Botswana.

Picha ya Ally Shatry, Afisa Habari Msaidizi wa Simba Sc

Katika mchezo wa ugenini uliopigwa Botswana wiki iliyopita ‘Wekundu wa Msimbazi’ walitanguliza mguu mmoja katika hatua ha makundi baada ya kuibuka na ushindi wa bao 2-0 yaliyofungwa na John Bocco na Tadeo Lwanga.