Kikosi cha Simba
Ikitoka kulikosakosa Kombe la Mapinduzi baada ya kufungwa 1-0 na Azam FC katika fainali usiku wa Ijumaa Uwanja wa Amaan, Zanzibar bao pekee la kiungo Himid Mao Mkami kwa shuti kali, Simba itajaribu kuendelea kufanya vizuri katika Ligi Kuu Jumatano.
Kwa sasa, Wekundu hao wa Msimbazi ndiyo wanaongoza Ligi Kuu kwa pointi zao 44 za mechi 18, wakifuatiwa na mabingwa watetezi, Yanga wenye pointi 40 za mechi 18 pia.