Jumatano , 21st Jun , 2017

Mfalme wa mashairi, Afande sele amewachana viongozi wa klabu za mpira wa bongo,(Simba na Yanga) kwamba haamini kama Tanzania nzima hakuna vijana wenye umri mdogo mpaka kuanza kugombea wachezaji wazee.

Afande amefunguka hayo kupitia ukurasa wake kijamii facebook baada ya mvutano wa vilabu vya mpira nchini kumgombea wachezaji wa kimataifa akiwamo raia wa Rwanda Nahodha Haruna Niyonzima, kabla klabu yake kuthibitisha kushindwana katika maslahi.

"Soka ni mchezo wa umri siamini kama bongo yote hakuna madogo wenye vipaji na nguvu za kuwashinda hawa vibabu tunaolazimishwa kuamini bado wapo kwenye viwango, soka la bongo ni sawa na soka la hongo, uozo na mizozo ndiyo nguzo na gumzo" aliandika Afande Sele