Jumanne , 1st Dec , 2020

Bingwa wa ulimwengu, Lewis Hamilton atakosa mashindano ya Formula 1 yajulikanayo kama Sakhir Grand Prix ya wikendi hii nchini Bahrain baada ya kukutwa na Covid-19.

Bingwa wa Dunia katika mbilo za langalanga, Lewis Hamilton akitabasamu baada ya ushindi.

Timu yake, Mercedes, ilisema Muingereza huyo aliamka na dalili za ugonjwa huo siku ya Jumatatu na akarudisha matokeo mazuri kwenye vipimo vya awali lakini akagundulika kuwa nao katika maaribuo ya pili.

Hamilton, ambaye sasa anajitenga mwenyewe, alishinda Bahrain Grand Prix katika mzunguko huo Jumapili iliyopita sasa atakosa mbio za Jumapili kwa mara ya kwanza tangu mchezo wake wa kwanza wa F1 kwenye mbio za ufunguzi wa msimu wa 2007 huko Australia.

Mbabe huyo mwenye umri wa miaka 35, alitwaa taji lake la saba linalofanana na rekodi katika ulimwengu wa Grand Prix ya Uturuki mnamo 15 Novemba.