Sports in brief
Timu ya soka ya Azam ya Dar es Salaam jana ilipanda kwa nafasi moja kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifunga JKT Oljoro mabao 3-0.
Mchezo huo ambao ulikuwa wa vuta nikuvute ulifanyika Uwanja wa Azam Chamazi, ambapo hadi mapumziko washindi walikuwa mbele kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na Mrisho Ngasa na John Bocco.
Wachezaji wa Oljoro ambao wiki iliyopita walifungwa mabao 2-0 na Simba walijaribu kutulia kipindi cha kwanza, lakini tatizo la umaliziaji lilikuwa kikwazo kikubwa kwao. Walipata nafasi kadhaa za kufunga, lakini ama walipiga nje ya lango au kupiga mashuti dhaifu yaliyodakwa na kipa wa Azam Mwadini Ally.
Print
More Sports in Brief
Prime Time
EATV Shows