Sports in brief
Yanga sasa imetamka rasmi kuwa inataka mechi yao na Zamalek katika Ligi ya Mabingwa Afrika iwe moja kwa sababu ya hali ya usalama nchini Misri si nzuri.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Yanga, Selestine Mwesigwa alisema jana kuwa wameandika barua Shirikisho la Soka nchini (TFF) wakiomba iwasilishe maombi yake kwenye Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kutaka wacheze mchezo mmoja badala ya miwili na Zamalek.
Alisema kanuni za mashindano ya Ligi ya Mabingwa zinatoa fursa ya kuwa na mchezo mmoja badala ya miwili utakaochezwa kwenye nchi ambayo amani yake ni ya uhakika na hivyo kulingana na hali halisi ya Misri kwa sasa wangetaka mchezo huo uchezwe Dar es Salaam.
Print
More Sports in Brief
Prime Time
EATV Shows