Sports in brief
Ofisi za Chama cha Gofu Tanzania (TGU) sasa zimehamia Klabu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Lugalo jijini kutoka Gymkhana Dar es Salaam (DGC).
Ofisa Tawala wa TGU, Sophie Nyanjera alithibitisha kuhama kwa ofisi hiyo Dar es Salaam jana. “Wapenzi, marafiki, vyombo vya habari na wadhamini, napenda kuwafahamisha kwamba ofisi zetu kuanzia Februari 7 mwaka huu zimehamia klabu ya Lugalo Dar es Salaam,” alisema Nyanjera.
Ofisa huyo alishukuru kwa msaada wote ambao alipata kwa wadau na kutarajia kuendelea hivyo watakapokuwa Lugalo. Tangu mwaka jana kumekuwa na mvutano katika Utawala wa DGC kuhusiana na uwepo wa ofisi ya TGU kwenye klabu hiyo kabla ya kufikia uamuzi wa kuwataka waondoke.
Print
More Sports in Brief
Prime Time
EATV Shows