Search

Sports in brief 

Simba wakwea pipa

Kocha mkuu wa vinara wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Simba, Mserbia, Milovan Circovic, ameanika kikosi cha wachezaji 18 ‘waliokwea pipa’ jana kwenda Kigali Rwanda tayari kwa mechi ya awali ya michuano ya Kombe la Shirikisho (CAF), dhidi ya Kiyovu inayotarajiwa kupigwa keshokutwa Stade De Journal.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema kikosi hicho cha Circovic, kimeondoka kikiwa na matumaini kibao ya kurudi na ushindi, baada ya mazoezi ya maangamizi kwa siku mbili kwa ajili ya kuwakabili Wanyarwanda hao.

Kamwaga, aliwataja wachezaji waliokwea pipa kuwa ni makipa Juma Kaseja na Ally Mustafa ‘Barthez’, mabeki wakiwa ni Juma Jabu, Said Nassor Cholo, Obadia Mungusa, Victor Costa, Juma Nyoso, Kelvin Yondani, huku viungo wakiwa ni Shomari Kapombe, Mwinyi Kazimoto, Patrick Mafisango, Jonas Mkude, Salum Machaku, Uhuru Selemani na Edward Christopher.

Washambuliaji ni Emmanuel Okwi, Felix Sunzu na Ramadhan Singano ‘Messi’, ambapo msafara wa wachezaji na viongozi takriban 22 ukiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange ‘Kaburu’, ulitarajiwa kutua jana usiku jijini Kigali kwa ndege ya Rwanda.

Print

 More Sports in Brief

Mwili wa kiungo wa kimataifa wa Simba na timu ya taifa ya Rwanda, Patrick Mutesa Mafisango, aliyefariki dunia jana alfajiri kwa ajali ya gari unatarajiwa kuagwa leo kwenye Uwanja TCC Sigara Chang'ombe more
Mchezaji wa Simba, Patrick Mutesa Mafisango (32) aliyefariki dunia jana alfajiri kwa ajali ya gari ataagwa leo kwenye Uwanja TCC Sigara Chang'ombe Jijini Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kuelekea nyumbani more
Mchezaji wa Kimataifa wa Klabu ya Simba, Patrick Mafisango amefariki dunia leo alfajiri kwa ajali ya barabarani wakati akijaribu kumkwepa mwendesha pikipiki katika eneo la Tazara JiJini Dar es Salaam. Kwa more
Chama cha Riadha nchini Tanzania (RT) kimetangaza majina ya wagombea wa nyadhifa mbali mbali za uongozi wa chama hicho kwenye uchaguzi mkuu ujao takao fanyika Mei 20 mwaka huu mkoani Moroggoro. Mwenyekiti more
Simba wanawasili nchini leo baada ya kutolewa katika mashindano ya Kombe la Shirikisho na Al Ahly Shandy ya Sudan, kwa matuta. Mwenyekiti wa Simba Aden Rage amesema baada ya kufika Dar es Salaam timu more
 Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji 25 tayari kujiandaa na mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia hatua ya makundi Kanda ya Afrika dhidi ya more
 Wawakilishi wa Tanzania katika mashindano ya Kombe la Shirikisho, Simba FC wameaga mashindano hayo baada ya kutolewa na Al Ahly Shandy kwa penati 9-8. Katika mechi hiyo iliyochezwa jana usiku nchini more
Timu ya Taifa ya Karate ya Tanzania imeibuka washindi katika michuano ya mabingwa wa Afrika iliyomalizika Jijini Kampala nchini Uganda. Katika michuano hiyo iliyodumu kwa wiki moja Tanzania ilifanyavyema more
Timu ya taifa ya wanawake ya Zimbabwe imewasili hii leo tayari kwa mchezo wa kujipima nguvu dhidi ya timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania ‘Twiga Stars,mchezo utakaopigwa  jumamosi ya mei 12 more
Timu ya taifa ya Tanzania ya netiboli, ‘Taifa Queens’ jana ilikutana na kisiki baada ya kukubali kulala kwa timu bora Afrika, Malawi, kwa magoli 34-30 katika mashindano ya Afrika yanayoendelea more
News Poll

 Prime Time

18 55
  KURASA
19 00
20 00
  URBAN HEAT
20 30
20 55
  MUHTASARI WA MICHEZO
21 00
  URBAN HEAT
22 30
  JUMP OFF
23 05
  CARIBBEAN HITS

 EATV Shows