Sports in brief
Kocha mkuu wa vinara wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Simba, Mserbia, Milovan Circovic, ameanika kikosi cha wachezaji 18 ‘waliokwea pipa’ jana kwenda Kigali Rwanda tayari kwa mechi ya awali ya michuano ya Kombe la Shirikisho (CAF), dhidi ya Kiyovu inayotarajiwa kupigwa keshokutwa Stade De Journal.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema kikosi hicho cha Circovic, kimeondoka kikiwa na matumaini kibao ya kurudi na ushindi, baada ya mazoezi ya maangamizi kwa siku mbili kwa ajili ya kuwakabili Wanyarwanda hao.
Kamwaga, aliwataja wachezaji waliokwea pipa kuwa ni makipa Juma Kaseja na Ally Mustafa ‘Barthez’, mabeki wakiwa ni Juma Jabu, Said Nassor Cholo, Obadia Mungusa, Victor Costa, Juma Nyoso, Kelvin Yondani, huku viungo wakiwa ni Shomari Kapombe, Mwinyi Kazimoto, Patrick Mafisango, Jonas Mkude, Salum Machaku, Uhuru Selemani na Edward Christopher.
Washambuliaji ni Emmanuel Okwi, Felix Sunzu na Ramadhan Singano ‘Messi’, ambapo msafara wa wachezaji na viongozi takriban 22 ukiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Simba, Godfrey Nyange ‘Kaburu’, ulitarajiwa kutua jana usiku jijini Kigali kwa ndege ya Rwanda.
Print
More Sports in Brief
Prime Time
EATV Shows