Anafahamika kama Bibi Cheka au Bi Cheka unaweza kumuita hivyo yote sawa,hiki ni kipaji kipya kwenye tasnia hii ya muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Fleva,kwa mara ya kwanza akutana uso kwa uso na Mh Temba mmoja kati ya wasanii wakongwe wa muziki wa Bongo Fleva hapa nchini Tanzania,ambae anatoka kwenye kundi kongwe pia la muziki wa Bongo Fleva Wanaume Family ambalo lipo chini ya Saidi Fella,
Bi Cheka na Mh Temba wamefanikiwa kupiga mkwaju mkali unaoitwa Ni wewe.Ni moja kati ya kazi ambazo inasemekana itakuja kufanya vizuri sana kwenye medani ya muziki huu wa Bongo Fleva.
Print
Comments
Next On:
EATV Shows