Jumanne , 11th Dec , 2018

Watu wawili wamefariki duniani Mkoani Morogoro baada ya mtu aliyedaiwa kuwa na ugonjwa wa akili kumuua ndugu yake na kisha yeye mwenyewe kujinyonga walipokuwa kwa mganga wa kienyeji kwaajili ya kupata matibabu.

Mauaji

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Polisi Wilbord Mtafungwa amesema kuwa tukio hilo limetokea desemba 1, 2018 baada ya Lucian Kigolo (54) ambaye anamatatizo ya akili kumshambulia kaka yake Gerald Kigolo(60) kwa kumpiga na kitu kizito kichwani.

Aidha Kamanda huyo amesema baada ya kutenda tukio hilo, mtu huyo aliamua kujinyonga kwa kutumia kamba  nyumbani kwa mganga wa kienyeji ambaye ametambulika kwa jina la Luka Paulo (50), ambapo katika tukio hilo Jeshi la Polisi linamshikilia mganga huyo.

Katika tukio lingine, jeshi la polisi linawashikilia watu watatu akiwemo Filbert Katabazi mkazi wa Dare s saalam kwa  tuhuma ya wizi wa mtandaoni,  baada ya kujipatia fedha kiasi cha sh 4,900,000 zisizo halali kwa kutumia njia ya mtandao.