Alhamisi , 22nd Feb , 2018

Chama cha Mapinduzi (CCM), Zanzibar kimesema kuwa kimepokea kwa mshtuko mkubwa sana juu ya kuendelea kwa wimbi kubwa la unyanyasaji wa kijinsia linaloendelea kwa kasi huko visiwani Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi wa chama hicho Zanzibar, Catherine Peter Naao, amevitaka vyombo vya dola kufanya operation maalumu juu ya matukio hayo ambayo kila siku yamekuwa yakichukua kasi kubwa sana.

Amesema chama hicho kinafahamu kuwa kwa Mkurugezi wa mashataka yapo mashataka zaidi ya 150 ya watu mbalimbali kuhusina na matuki hayo, lakini bado hayajapelekwa mahakamani hivyo ameomba wajitahidi kukamailisha uchunguzi na taratibu kwa haraka ili jamii iweze kuona namna ya matukio hayo yanavyoweza kukomeshwa.

Aidha amesema Chama cha Mapinduzi ambacho ndio wasimamizi wa ilani ya uchaguzi ya CCM kinaona kwamba lazima kuongezwe kasi ya usimamizi kwa kuwakumbusha kuwa Chama pamoja na jamii inakerwa na matukio hayo.