Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.
Dkt Kikwete ameyabainisha hayo leo Mei 30, 2020, jijini Dodoma, wakati wa zoezi la kukabidhiwa ndege aina ya Tausi kwa Marais wastaafu pamoja na mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere.
"Mimi ndiyo mdogo nasema kwa niaba ya Wazee hawa, tunatoa shukrani kwa moyo wako wa upendo kwa kutupatia hawa ndege, tulikuwa tunawatamani lakini ukitoka nao, ukafika nao Msoga, watu watasema amepora, pia nakupongeza kwa maamuzi ya incubator lakini yule Msukuma sikukuambia umfukuze, lakini nilieleza tu masikitiko yangu" amesema Dkt Kikwete.
Aidha awali wakati akizungumza, Rais Magufuli amewapongeza Marais wote Wastaafu walioshiriki kuwatunza Tausi hao.