Jumanne , 22nd Jan , 2019

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda na Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima wamekutana uso kwa uso katika mkutano wa kisekta wa Wizara ya Madini.

Josephat Gwajima (kushoto) na Paul Makonda (kulia)

Katika mkutano huo unaofanyika katika ukumbi wa JNICC Jijini Dar es salaam , RC Makonda alimsimamisha Askofu Gwajima Mbele ya Rais John Pombe Magufuli ambae ni mgeni rasmi.

"Nimemuona rafiki yangu Gwajima hapa, simama kidogo wakuone", amesema Makonda na baada ya Askofu Gwajima kusimama, ukumbi mzima ulikaripuka kwa shangwe.

"Mimi na yeye tuna historia ndefu kidogo, wameninoa wengi kuanzia enzi za umoja wa vijana, kwa hiyo kama kuna mapambano, unaweza kunituma tu", ameongeza Makonda.

Ikumbukwe kuwa wawili hao walizua gumzo mwanzoni mwa mwaka uliopita kutokana na suala la uhalali wa elimu ya Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es salaam, ambapo Askofu Gwajima alitumia mikutano yake mingi kuelezea jinsi alivyokuwa akimfahamu.