Jumatano , 18th Mar , 2020

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa idadi ya wagonjwa wa Virusi vya Corona nchini imeongezeka na kufikia watatu, ambapo mmoja amepatikana Zanzibar ambaye ni Mjerumani, mwingine Jijini Dar es Salaam ambaye ni Mmarekani

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu ameagiza pia Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari ya ugonjwa huo, na kwamba Serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kusitisha baadhi ya shughuli na kwamba maduka na masoko na shughuli za usafirishaji zitaendelea na hakuna umuhimu wa kujaza abiria kwa kipindi hiki.

"Tayari wagonjwa wawili wamepatikana wa maambukizi ya Virusi vya Corona, mmoja kutoka Zanzibar, sampuli zake zililetwa maabara kuu yeye ni Mjerumani (24), yuko kwenye uangalizi, hapa Dar es Salaam tuna Mmarekani (61), na tutaendelea kuwahifadhi hawa hadi tukapojiridhisha tatizo limekwisha basi tutaweza kuwaondoa" amesema Waziri Mkuu.