Kamanda Lazaro Mambosasa
Akiongea na www.eatv.tv Kamanda Mambosasa, amesema taarifa hizo zipo, na wao kama jeshi la Polisi wanaendelea kufuatilia kwa karibu.
''Ni kweli taarifa zipo zinasambaa na sisi tunafuatilia, watu watulie tu kwasababu unaweza ukakuta mtu mmoja tu ameanzisha'', Mambosasa.
Aidha kabla ya kuongea na Mambosasa, www.eatv.tv ilimtafuta Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni, (ACP) Mussa Taibu ambaye aliweka wazi kuwa wamejipanga na kuimarisha usalama.
''Tumejipanga na vikosi vyetu kama kawaida kuhakikisha tunaimarisha usalama wetu na tunahakikisha maeneo yote yana usalama wa kutosha na sio wka hili tu, muda wote vikosi vyetu vipo tayari'', amesema Kamanda Taibu.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ubalozi wa Marekani, maeneo yanayohofiwa huenda shambulio likafanyika ni Masaki katika hoteli na migahawa.