Ijumaa , 23rd Mar , 2018

Mkuu wa Oparesheni maalum za Kipolisi Liberatus Sabas amesema jeshi la polisi litaendelea na ya kukabiliana na mtandao wa dawa za kulevya Zanzibar itaendelea sambamba na kuwadhibiti wahalifu wanaofanya vitendo vya kuwaibia na kuwadhuru watalii.

Kamanda Sabas amesema wataendeleza operation hizo mpaka wahalifu watakaposema wamesalimu amri katika kufanya vitendo hivyo.

Aidha amesema kwa upande wa dawa za kulevya wamegundua wapo wafanyabiashara Zanzibar wanaoshirikiana na wale wa Tanzania bara na kuhakikisha kwamba watawashughulikia na kisha kuwafikisha katika mikono ya sheria na kusisitiza kuwa hakuna atakayechomoka.

Aidha imedaiwa kwatika Oparesheni hizo wamekamatwa wahalifu wapatao 21 pamoja na kete za dawa za kulevya kete 695 zenye ujazo takribani 31.3 gram.