Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola.
Akizungumza na wanahabari leo Oktoba 16, Lema amesema kuwa kitendo cha waziri Lugola kuzuia watu kuzungumzia matukio ya utekwaji wa watu yanayojitokeza kwa sasa hapaswi kufanya hivyo badala yake ni kung'atuka ili kupisha kashfa.
Lema amesema kuwa serikali inatakiwa kuviruhusu vyombo vya ulinzi vya kimataifa kuisaidia Tanzania na kuchunguza mfululizo wa matukio hayo yakiwemo ya kushambuliwa kwa Lissu na kupotea kwa mwanahabari.
"Waziri wa mambo ya ndani kakiri kwamba utekaji umekuwepo, na kuna watu wametekwa, na kuna watu wametoweka, ukiwa na hekima unang'atuka, tunaitaka serikali ifanye kila liwezekanalo mara moja kuhakikisha vyombo vya upelelezi vya kimataifa vinatupatia msaada kwenye hili haraka iwezekanavyo", amesema Lema.
Akizungumza na wanahabari Jumamosi Oktoba 13, Waziri Lugola alisema kuwa matukio ya utekwaji wa watu nchini tangu mwaka 2016 ni watu 75 walitekwa huku wengine wakipatikana wakiwa hai na wengine kutopatikana kabisa.